Friday, July 20, 2012

Yah.kula daku mwezi huu wa Ramadhan,Daku unaweza kula saa yote hadi inapoingia...

Daku unaweza kula saa yote hadi inapoingia Alfajiri. Hii ni kutoka na kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

((..وَكُلُواْ وَاشْرَبُواْ حَتَّى يَتَبَيَّنَ لَكُمُ الْخَيْطُ الأَبْيَضُ مِنَ الْخَيْطِ الأَسْوَدِ مِنَ الْفَجْرِ ثُمَّ أَتِمُّواْ الصِّيَامَ إِلَى الَّليْلِ...))

((…Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa alfajiri katika weusi wa usiku. Kisha timizeni Swawm mpaka usiku…)) [Al-Baqarah: 187]

Hivyo, unaruhusiwa kula daku hadi Alfajiri ndipo unapoanza kufunga. Na hata Muadhini akiadhini na kama una tonge au fundo la maji mdomoni usiliteme, kamilisha kulimeza kisha ndio uanze kufunga. Haya yamethibiti katika Sunnah kama inavyoonyesha Hadiyth ifuatayo:

عن ابن عمر رضي الله عنهما قال: كان لرسول الله صلى الله عليه وسلم مؤذنان:
بلال وابن أم مكتوم .فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم ((إن بلال يؤذن بليل
فكلوا واشربوا حتى يؤذن ابن أم مكتوم)) متق عليه

Kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhuma) ambaye amesema: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa na waadhini wawili; Bilaal na Ibn Ummi Maktuum. Akasema: ((Hakika Bilaal anaadhini usiku (adhana ya mwanzo), basi kuleni na mnywe hadi aadhini Ibn Ummi Maktuum)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

Na Allaah Anajua zaidi

Kujihifadhi ni Miongoni mwa sifa Alizozitaja za mwanamke na si tu kwa mwezi huu mtukufu wa Ramadhan

Kujihifadhi ni Miongoni mwa sifa Alizozitaja za Mwanamke Allaah
(Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema:

Na waambie Waumini wanawake wainamishe macho yao, na wazilinde tupu
zao, wala wasionyeshe uzuri wao isipokuwa unaodhihirika. Na waangushe
shungi zao juu ya vifua vyao, wala wasionyeshe uzuri wao ila kwa waume
zao, au baba zao, au baba wa waume zao, au watoto wao, au watoto wa
waume zao, au kaka zao, au... wana wa kaka zao, au wana wa dada zao,
au wanawake wenzao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, au wafuasi
wanaume wasio na matamanio, au watoto ambao hawajajua mambo
yaliyokhusu uke. Wala wasipige chini miguu yao ili yajulikane mapambo
waliyoyaficha. Na tubuni nyote kwa Allah enyi Waumini, ili mpate
kufanikiwa.

Hivyo ni vyema kujisitiri wakati wote ma si tuu mwezi wa Ramadhan au siku ya ijumaa kama wafanyavyo baadh ya akina mama na akina dada

Fadhila za kuswali jamaa alfajiri na kumsabihi All mpaka jua lichomoze hasa mwezi huu Mtukufu wa RAMADHANI

عن أنس عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنه قال (( من صلى الفجر في جماعة ثم قعد يذكر الله حتى تطلع الشمس ثم صلى ركعتين كانت له كأجر حجة وعمرة تامة تامة تامة) ) أخرج الترمذي صححه الألباني .

Imetoka kwa Anas kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Atakayeswali Alfajiri katika Jama'ah kisha akakaa anamkumbuka Allaah mpaka likachomoza jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio kamili kamili kamili)) [Imetolewa na At-Tirmidhiy na kaisahihisha Al-Albaaniy]

Pindi ukifanya hivyo kwa mwezi mzima utakuwa umechuma thawabu za Hajj na 'Umrah mwezi mzima. Hizo ni fadhila za siku za kawaida, seuze ukifanya mwezi mtukufu huu wa Ramadhaan? Jitahidi ndugu Muislamu kadiri uwezavyo kuchuma hizi thawabu kubwa ambazo zingelikukalifu mali, tabu za safari na mashaka ya kufika Makkah kutekeleza ibada hizo. Lakini kwa Rahma ya Allaah Ametujaalia tuweze kuzichuma tukiwa majumbani mwetu tena kwa wepesi kabisa. Wanaume thawabu zitazidi ikiwa watatekeleza wakiwa misikitini. Wanawake wanazipata fadhila hizo hata wakiswali majumbani mwao. Hata hivyo, pamoja na ujira wote huu, tusisahau kuwa fadhila hizo hazivunji wala hazifuti fardh ya kwenda Hajj kwa mwenye uwezo, asije mtu akadhani kufanya hayo kutakuwa kumetengua wajiibu wake wa kuhiji au kufanya 'Umrah.

Saturday, July 7, 2012

Alhamdulillah neno "vunja jungu" limetokomea...ambalo hutokea kabla ya mwezi wa Ramadhani kwa kuingza watu madisko

Alhamdulillah neno "vunja jungu" limetokomea ndani ya manispaa ya morogoro kwa takriban miaka 4 sasa.
---------------------------------------
Kama tunavyofahamu kuwa inapokaribia mwezi wa ramadhan kawaida huwa kunakuwa na matangazo ya madisco na taarab ,katika matangazo hayo huwa linaandikwa neno vunja jungu.
Hii kwa mazoea kuwa mwezi wa tawba umefika hivyo watu wanakumbushwa wamalizie yale maasi kabla mwezi kuingia,au kwa lugha nyingine kuwa ni wito kwa waislaam kufanya maasi kabla ramadhan kuingia.

Na pia zinapokaribia sikukuu zetu za eid huwa matangazo kama haya yanaonekana mitaanai "disco baab kubwa la eid alhajj au eid el fitr"

Hii ni kudhalilisha dini yetu na kuikashif.

Nani wakulamiwa?

Wakulaumiwa ni manispaa idara ya matangazo ambayo inatoa ruhusa hio,kwani huruhusiwi kutoa tangazo lolote bila kuomba kibali manispaa na kulipia.

Wapili kulaumiwa ni waislam wenyewe kukaa kimya bila kudai haki yao.

Kwanini Manispaa ya morogoro imefanikiwa?

Hii ni baada ya waislam kulalamika na kuomba haki yao.

Zipi njia za kufanya ili kuipata haki hio?

Kwanza kabisa tufahamu kuwa nchi yetu si ya kiislaam na inatawalia kisheria na kanuni.

Na pia nchi yetu inadaiwa kuwa haina dini bali inaheshimu dini zote.

Pia kuifahamisha serikali kwa njia ya mdomo na maandishi kuwa hilo jambo ni tusi kwenye dini yetu hivyo kuomba msaada wa serikali kutatua tatizo hilo.

Zifuatazo ni njia sahihi za kuomba haki hizo.

1.Kuunda kamati itakayofuatilia Jambo hilo na kuhusisha taasisi za kiislam zilizopo katika eneo husika,au kuhusisha mtu mmoja mmoja kutoka kila taasisi (bakwata msiwasahau sometimes wanasave :). )

2.Kuwafahamisha wailsam juu ya qadhia hio ili waiunge mkono.

3.Kuiomba serikali (mkurugenzi wa manispaa) isaidie kupiga marufuku jambo hilo na mumfahamishe kwa njia nzuri kuwa jambo hilo ni kukashifiwa kwa dini ya kiislam.

4.Majadiliano yote yawe kwa maandishi na msikubli kujibiwa na midomo lazima kwa maandishi.na kopi ziende kwa rpc na mkuu wa mkoa.

5.Kukumbushia kila wakati majibu hayo kwani kiuzoefu hua yanachelewa sana inaweza kuchukua zaidi ya mwaka.

6.kufanya kazi hio kwa ikhlaas na kuwa na subra kwa yatakayojitokeza.

7.Kuacha kutumia jazba bila kutoa elimu ya jambo hilo kwa serikali.

Nini chakufanya baada ya kupata haki hio?

Kila inapokaribia mwezi wa ramadhan au eid niwajib kuikimbusha serikali kwa barua kuwa ramadhan au eid zinakaribia hivyo kuwakumbusha wale wote wanaokuja kuchukua kibali cha madisco wasihusishe miezi au sikukuu zetu.

Baada ya hapo kila muislam atakae ona tangazo baso ahakikishe analiondoa kwa mkono wake.

Na ushindi unatoka kwa Allah pekee

Darsa la maandalizi ya mwezi wa Ramadhani

ASSALAAMU 'ALAYKUM WARAHMATULLAAHI WABARAKAATUH

DARASA LA MAANDALIZI YA MWEZI WA RAMADHANI.

Ndg zangu ktk imaan ktk darasa letu la sehemu ya kwanza tuliangalia baadhi ya mambo kama nguzo za funga,masharti yake,sunnah zake nk:

Ktl sehemu hii ya pili tutaangalia maaswi ya viungo vyote vya mwili ambavyo vinampelekea mja ktk kuiharibu funga yake.

MAASWI YA VIUNGO.

Maswi ya viungo ni maaswi yote ya tumbo. mfano:- kula riba,kunywa kila chenye kulewesha,kula mali ya mayatima,na kila kile ambacho amekiharamisha juu m/mungu juu yake miongoni mwa vyenye kuliwa na kunywewa,na hakika amemlaani m/mungu na mtume wake mwenye kula riba na kila mwenye kusababisha juu ya kula kwake,

na amemlaani m/mungu mwenye kunywa pombe na kila mwenye kusababisha kunywa kwake mpaka mpikaji,muuzaji,mbebaji nk.

Ktk post zijazo in shaa allaah tutaangalia kiungo kimoja kimoja pamoja na maaswi yake ili tuwe navyo makini visije vikawa ni sababu ya kuharibu funga zetu. wallaahu a'alam.

Kwanini tunafunga SWAUMU,soma kwa faida

((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ كُتِبَ عَلَيْكُمُ الصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكُمْ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ)) (( أَيَّامًا مَّعْدُودَاتٍ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ وَعَلَى الَّذِينَ يُطِيقُونَهُ فِدْيَةٌ طَعَامُ مِسْكِينٍ فَمَن تَطَوَّعَ خَيْرًا فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ وَأَن تَصُومُواْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ)) ((شَهْرُ رَمَضَانَ الَّذِيَ أُنزِلَ فِيهِ الْقُرْآنُ هُدًى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَاتٍ مِّنَ الْهُدَى وَالْفُرْقَانِ فَمَن
شَهِدَ مِنكُمُ الشَّهْرَ فَلْيَصُمْهُ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوْ عَلَى سَفَرٍ فَعِدَّةٌ مِّنْ أَيَّامٍ أُخَرَ يُرِيدُ اللّهُ بِكُمُ الْيُسْرَ وَلاَ يُرِيدُ بِكُمُ الْعُسْرَ وَلِتُكْمِلُواْ الْعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُواْ اللّهَ عَلَى مَا هَدَاكُمْ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ))

((Enyi mlioamini! Mmefaradhishiwa Swawm, kama waliyofaradhishiwa waliokuwa kabla yenu ili mpate kumcha Allaah))(([Mfunge] siku maalumu za kuhisabika. Na atakayekuwa miongoni mwenu mgonjwa au yumo safarini basi atimize hisabu katika siku nyengine. Na wale wasioweza, watoe fidiya kwa kumlisha masikini. Na atakayefanya wema kwa kujitolea, basi ni bora kwake. Na mkifunga ni bora kwenu, kama mnajua)) ((Mwezi wa Ramadhaan ambao imeteremshwa humo Qur-aan kuwa ni uongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongofu na upambanuzi. Basi atakayekuwa mjini katika mwezi huu na afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Allaah Anakutakieni yaliyo mepesi wala Hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Allaah kwa kuwa Amekuongoeni ili mpate kushukuru))